![]() |
Rais Mugabe hupinga sana wapenzi wa jinsia moja |
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe
alikutana na Askofu mkuu wa Canterbury na kuibua maswali kuhusu ndoa za wapenzi
wa jinsia moja.
Askofu mkuu Justin Welby amesema
alimjibu kiongozi huyo kwamba kuna mitazamo tofauti kuhusu ndoa hizo miongoni
mwa waumini wa kanisa la Kianglikana kote duniani.
Aliongeza hata hivyo kwamba wengi wa
waumini wanaamini ndoa ni uhusiano wa muda mrefu baina ya mwanamume na
mwanamke.
Askofu Welby alisema ni makosa
kuwahukumu au kuwaadhibu watu kwa sababu ya msimamo wao kijinsia na kimapenzi.
Hata hivyo, amesema dalili
zilionesha Bw Mugabe hakukubaliana naye.
“Sidhani itakuwa haki kusema kwamba
Bw Mugabe alikubaliana nami kabisa,” alisema Askofu Welby.
Mkutano huo wa faraghani ulifanyika
mjini Harare, baada ya Askofu Welby, ambaye yumo katika taifa jirani la Zambia
anakohudhuria mkutano wa viongozi wa kanisa la Kiangilikana kufanya ziara fupi
Zimbabwe.
Msemaji wa Lambeth Palace amesema
mpango huo ulipangwa dakika za mwishomwisho na ulidumu chini ya saa moja.
Bw Mugabe ni Mkatoliki na hupinga
sana ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
![]() |
Askofu Welby amesema Bw Mugabe hakukubaliana naye kabisa |
Maafisa wa kanisa hilo wamesema
mkutano huo ulikuwa sana wa kidini badala ya kisiasa ingawa uhusiano baina ya
serikali na kanisa ulijadiliwa.
No comments:
Post a Comment