Saturday, February 27, 2016

Mwalimu Christopher Sign kutoka Uingereza akitoa shukrani zake za dhati wakati wa hafla fupi ya kumuaga katika Chuo cha Habari Maalum.

Mkuu wa Chuo Cha Habari Maalum kushoto na Mwalimu Christopher Sign, Picha na Grace Lawi.

Picha ya pamoja baada ya kumaliza Course ya Writing for Media na mwalimu Christopher Sign.

                  Wanafunzi wa Diploma mwaka wa kwanza katika picha na mwalimu wao Bwn, Christopher Sign.                                 Picha na Grace Lawi


Umoja wa wanafunzi wa chuo cha Habari Maalum watembelea kituo cha watoto yatima Yeriko kilichopo Ngaramtoni Arusha.



Umoja wa wanafunzi wa chuo cha Habari Maalum watembelea kituo cha watoto yatima Yeriko kilichopo Ngaramtoni Arusha.

Na Grace Lawi,



Wanafunzi wa chuo cha Habari Maalum wamewatembelea watoto yatima katika moja ya vituo vya watoto yatima.


Hayo yamesemwa na Rais wa chuo Bwn, Wilfred Mikomangwa alipokuwa akiwashukuru wanafunzi hao kwakuonyesha juhudi zao katika swala hilo, wakati wa ibada fupi ya jioni chuoni hapo.
Watoto wa Kituo Cha Yeriko. Picha na Grace Lawi.

Wanafunzi hao wameonyesha muhamko mkubwa sana juu ya swala hili kwani kila ifikapo mwisho wa mwezi kiwango cha utoaji kinaungezeka maradufu.

Aidha, waalimu wachuo hicho hawapo nyuma kuonyesha ushirikiano wao na wanafunzi katika kufanikisha swala hilo.


Hata hivyo, Serekari ya wanafunzi katika chuo hicho, wamekuwa bega kwa bega na wanafunzi hao na kuonyesha mfano mzuri, katika kuchangia pia na kwenda kuwatembelea watoto hao.


News



ZIARA YA SEREKALI  KATIKA CHUO CHA HABARI MAALUM ARUSHA

Na Grace lawi,

Uongozi wa chuo cha Habari Maalum umepongezwa kwaufanisi na jitihada katika kuboresha taaluma kwa nadharia na vitendo katika vitengo vyake.

Hayo yamesemwana Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Bwana Elisha Nkhambaku,  alipotembelea  chuo hicho nakuzungumza na uongozi wa chuo kuhusu maendeleo ya taaluma chuoni hapo.

Naye Mkuu wa chuo hicho bwana Jackson Kaluzi, amebainisha mafanikio yaliyofikiwa kuwa nipamoja  na wanafunzi  waliohitimu mwaka jana baadhi yao kupata kazi katika kituo cha habari cha star tv kilichopo mkoani Mwaza baada ya kufanya vizuri katika mazoezi kwa vitendo.

Aidha, Bwana Kaluzi ameelezea changamoto kubwa chuoni hapo kuwa nipamoja na uhaba wa wanafunzi kwani chuo hicho kina uwezo wakuchukua wanafunzi zaidi ya mia mbili.

Sanjarinahayo, Bwana Nkhambaku, ameahidi kuwabega kwa bega na chuo kwa kutangaza chuo hicho ili kupata wanafunzi wengi zaidi katika vitengo vya habari na mawasiliano pamoja na uongozi na utawala.