Saturday, February 27, 2016

News



ZIARA YA SEREKALI  KATIKA CHUO CHA HABARI MAALUM ARUSHA

Na Grace lawi,

Uongozi wa chuo cha Habari Maalum umepongezwa kwaufanisi na jitihada katika kuboresha taaluma kwa nadharia na vitendo katika vitengo vyake.

Hayo yamesemwana Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Bwana Elisha Nkhambaku,  alipotembelea  chuo hicho nakuzungumza na uongozi wa chuo kuhusu maendeleo ya taaluma chuoni hapo.

Naye Mkuu wa chuo hicho bwana Jackson Kaluzi, amebainisha mafanikio yaliyofikiwa kuwa nipamoja  na wanafunzi  waliohitimu mwaka jana baadhi yao kupata kazi katika kituo cha habari cha star tv kilichopo mkoani Mwaza baada ya kufanya vizuri katika mazoezi kwa vitendo.

Aidha, Bwana Kaluzi ameelezea changamoto kubwa chuoni hapo kuwa nipamoja na uhaba wa wanafunzi kwani chuo hicho kina uwezo wakuchukua wanafunzi zaidi ya mia mbili.

Sanjarinahayo, Bwana Nkhambaku, ameahidi kuwabega kwa bega na chuo kwa kutangaza chuo hicho ili kupata wanafunzi wengi zaidi katika vitengo vya habari na mawasiliano pamoja na uongozi na utawala.


No comments:

Post a Comment