Wednesday, July 20, 2016

Donald Trump kugombea urais Marekani


Donald Trump
DONALD TRUMP ameteuliwa rasmi  kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama cha REPUBLICAN,mara baada ya uungwaji mkono na wajumbe kutoka majimbo na wilaya za Marekani katika kura mchujo iliyofanyika  mjini CLEVELAND.

TRUMP ameuambia mkutano wa kitaifa wa chama cha Rebuplican kwamba anajivunia kuwa mgombea wa chama hicho katika uchaguzi wa urais mwezi Novemba mwaka huu na atashinda kura hiyo ili kuleta mabadiliko halisi kwa Washington.

Naye Spika wa bunge la wawakilishi, PAUL RYAN ameomba wajumbe kwenye kikao hicho kumuunga mkono TRUMP akieleza kuwa kutakuwa na uhakika wa ushindi iwapo tu wanachama wote wa Republican watashirikiana.
Chanzo BBC.

No comments:

Post a Comment