Wednesday, July 20, 2016

May kukutana na Merkel Ujerumani

May amemrithi David Cameron aliyejiuzulu baada ya kura ya maoni
 Waziri mkuu mpya wa Uingereza Theresa May leo amepangiwa kufanya ziara yake ya kwanza ng’ambo kama waziri mkuu ambapo ataelekea mjini Berlin, Ujerumani kukutana na kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Viongozi hao wawili watajadili utaratibu wa Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya baada ya raia nchini humo kuidhinisha hatua hiyo kwenye kura ya maoni mwezi uliopita.
Kadhalika, watajili uhusiano wa kibiashara wa siku zijazo.



Bi Merkel amekuwa na ushawishi mkubwa Ulaya
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier, amesema anatarajia Uingereza kuchukua hatua haraka kumaliza hali ya sintafahamu ambayo imetanda tangu kufanyika kwa kura ya maoni Uingereza.
Waandishi wa habari wanasema kuanzisha uhusiano wa moja kwa moja baina yake na Bi Merkel       litakuwa jambo muhimu sana kwa Bi May anapojaribu kufanikisha mazungumzo ya kuwezesha Uingereza kujiondoa vyema kutoka kwa EU.

Chanzo BBC

No comments:

Post a Comment