Thursday, July 21, 2016

Tahadhari mpya ya kiusalama yatangazwa nchini UTURUKI



Na Grace Lawi
Maelfu ya wananchi wanaokubaliana na msimamo wa serikali ya UTURUKI wamekusanyika  katika viwanja vya KIZILAY mjini ANKARA kuunga mkono kauli ya RAIS RECEP TAYYIP ERDOGAN kuhusu tahadhari mpya ya kiusalama nchini humo.

Mmoja wa viongozi wanaoiunga mkono serekali amesema wanakubaliana na   msimamo wa RAIS ERDOGAN  na kwamba watafanya lolote atakalosema kwakua yeye ndie mtu wanayemwamini na kumfuata.

Tayari  tahadhari zinaendelea kuchukuliwa kwa washukiwa wakijeshi na waungaji mkono wa mapinduzi katika maeneo mbalimbali nchini humo huku takwimu zikionyesha takribani watu elfu sitini  wamekamatwa au kutiwa hatiani.

No comments:

Post a Comment