Thursday, July 21, 2016

Kijana mweusi amefariki mikononi mwa polisi UFARASA


Polisi wakikabiliana na waandamanaji awali mjini Paris
 Na Grace Lawi
 Waandamanaji wameungana kukabiliana na maafisa wa polisi katika mji wa BEAUMONT-SUR-OISE huko UFARASA  baada ya kijana mweusi kufariki akiwa kizuizini.

Mabomu ya petroli yamerushwa na maafisa wa polisi na taarifa zinasema waandamanaji walijaribu kuteketeza ukumbi wa mji huku watu wanne wamekamatwa na kuzuiliwa.

Polisi wanasema Adama Traore alipata mshtuko wa moyo Jumanne baada yake kuzuiliwa katika mji huo ulioko kilomita thelathini kaskazini mwa Paris.

Lakini marafiki zake wanasema alikuwa buheri wa afya kabla ya kukamatwa na kwamba alipigwa na maafisa hao wa polisi hata hivyo uchunguzi wa kubaini chanzo cha kifo chake utafanywa baadaye Alhamisi.

Miaka 11 iliyopita, vifo vya vijana wawili waliokuwa wakijaribu kukwepa kukamatwa vilisababisha maandamano yaliyodumu wiki mbili katika viunga vya mji wa Paris na miji mingine nchini humo.

Tahadhari mpya ya kiusalama yatangazwa nchini UTURUKI



Na Grace Lawi
Maelfu ya wananchi wanaokubaliana na msimamo wa serikali ya UTURUKI wamekusanyika  katika viwanja vya KIZILAY mjini ANKARA kuunga mkono kauli ya RAIS RECEP TAYYIP ERDOGAN kuhusu tahadhari mpya ya kiusalama nchini humo.

Mmoja wa viongozi wanaoiunga mkono serekali amesema wanakubaliana na   msimamo wa RAIS ERDOGAN  na kwamba watafanya lolote atakalosema kwakua yeye ndie mtu wanayemwamini na kumfuata.

Tayari  tahadhari zinaendelea kuchukuliwa kwa washukiwa wakijeshi na waungaji mkono wa mapinduzi katika maeneo mbalimbali nchini humo huku takwimu zikionyesha takribani watu elfu sitini  wamekamatwa au kutiwa hatiani.

Chanjo dhidi ya HIV kufanyiwa majaribio Afrika


       Maendeleo kwenye chanjo ya HIV ndio suala kuu katika mkutano wa dunia wa ukimwi. Mtaalam wa juu wa ukimwi anasema hawezi kusema lini tiba ya HIV na Ukimwi huwenda ikaptiakana, lakini anasema amefurahishwa na maendeleo yake.

    Wanasayansi wanaohudhuria mkutano wa 21 wa kimataifa wa Ukimwi mjini Durban Afrika kusini wanasema bado hakuna chanjo ya kuzuia maambukizo ya HIV na ukimwi.

    Mkurugenzi wa taasisi ya kitaifa ya kimarekani ya afya na magonjwa ya kuambukiza Dr Anthony Fauci, anasema ni vigumu kutabiri pale chanjo dhidi ya HIV na ukimwi itapatikana, lakini anasema anamatumaini kuwa wanakaribia kupata tiba.

    Japo hakuna chanjo maalum ambayo imeonyesha matumaini, lakini wanayasayansi wanaendelea kwa dhati na majaribio ya chanjo HVTN 702.

    Chanjo hio inayofanyiwa majaribio ilitokana na majaribio yalofanywa nchini Thailand miaka michache ilopita na inaonyesha kiwango fulani cha ufanisi.

    Majaribio ya chanjo hiyo yanategemewa kuanza huko Afrika kusini na katika baadhi ya mataifa mengine ya Afrika baadae mwaka huu, lakini Dr. Fauci amesema itachukuwa muda kabla matokeo kupatikana.

Wednesday, July 20, 2016

Donald Trump kugombea urais Marekani


Donald Trump
DONALD TRUMP ameteuliwa rasmi  kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama cha REPUBLICAN,mara baada ya uungwaji mkono na wajumbe kutoka majimbo na wilaya za Marekani katika kura mchujo iliyofanyika  mjini CLEVELAND.

TRUMP ameuambia mkutano wa kitaifa wa chama cha Rebuplican kwamba anajivunia kuwa mgombea wa chama hicho katika uchaguzi wa urais mwezi Novemba mwaka huu na atashinda kura hiyo ili kuleta mabadiliko halisi kwa Washington.

Naye Spika wa bunge la wawakilishi, PAUL RYAN ameomba wajumbe kwenye kikao hicho kumuunga mkono TRUMP akieleza kuwa kutakuwa na uhakika wa ushindi iwapo tu wanachama wote wa Republican watashirikiana.
Chanzo BBC.

May kukutana na Merkel Ujerumani

May amemrithi David Cameron aliyejiuzulu baada ya kura ya maoni
 Waziri mkuu mpya wa Uingereza Theresa May leo amepangiwa kufanya ziara yake ya kwanza ng’ambo kama waziri mkuu ambapo ataelekea mjini Berlin, Ujerumani kukutana na kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Viongozi hao wawili watajadili utaratibu wa Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya baada ya raia nchini humo kuidhinisha hatua hiyo kwenye kura ya maoni mwezi uliopita.
Kadhalika, watajili uhusiano wa kibiashara wa siku zijazo.



Bi Merkel amekuwa na ushawishi mkubwa Ulaya
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier, amesema anatarajia Uingereza kuchukua hatua haraka kumaliza hali ya sintafahamu ambayo imetanda tangu kufanyika kwa kura ya maoni Uingereza.
Waandishi wa habari wanasema kuanzisha uhusiano wa moja kwa moja baina yake na Bi Merkel       litakuwa jambo muhimu sana kwa Bi May anapojaribu kufanikisha mazungumzo ya kuwezesha Uingereza kujiondoa vyema kutoka kwa EU.

Chanzo BBC

Wednesday, April 20, 2016

Trump na Clinton washinda New York


Furaha ya ushindi mjini New York

Zaidi ya nusu ya kura zilizohesabiwa katika uchaguzi wa awali wa urais nchini marekani katika mji wa New york,zinaonesha kwamba Donald Trump na Hillary Clinton wamepata ushindi mkubwa Zaidi ndani ya vyama vyote viwili.

Hillary Clinton ambaye amemshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa ameeleza katika hotuba yake kuwa ushindi wa chama chake cha Democratic umeweza kuwaunganisha zaidi wapinzani wake kuwa wamoja Zaidi ya kuwagawa.

Hata hivyo New York inatajwa kuwa ngome nyingine ya Donald Trump,ambapo Cruz yeye hesabu za kura zake zimeonekana kugoma mapema kabisa katika chama chake cha Repubilcan .

Wakati Hillary Clinton amemshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa .Hillary amewaambia wapinzani wake kuwa kuna la ziada linalowafanya wawe wamoja Zaidi ya kuwagawa.

Chanzo BBCswahili.
 

Tuesday, April 19, 2016

Grace lawi Jackson: Mugabe amlalamikia askofu kuhusu ndoa za jinsia mo...

Grace lawi Jackson: Mugabe amlalamikia askofu kuhusu ndoa za jinsia mo...: Rais Mugabe hupinga sana wapenzi wa jinsia moja   Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe alikutana na Askofu mkuu wa Canterbury na kuibua m...

Mugabe amlalamikia askofu kuhusu ndoa za jinsia moja


Rais Mugabe hupinga sana wapenzi wa jinsia moja

 Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe alikutana na Askofu mkuu wa Canterbury na kuibua maswali kuhusu ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Askofu mkuu Justin Welby amesema alimjibu kiongozi huyo kwamba kuna mitazamo tofauti kuhusu ndoa hizo miongoni mwa waumini wa kanisa la Kianglikana kote duniani.

Aliongeza hata hivyo kwamba wengi wa waumini wanaamini ndoa ni uhusiano wa muda mrefu baina ya mwanamume na mwanamke.

Askofu Welby alisema ni makosa kuwahukumu au kuwaadhibu watu kwa sababu ya msimamo wao kijinsia na kimapenzi.

Hata hivyo, amesema dalili zilionesha Bw Mugabe hakukubaliana naye.

“Sidhani itakuwa haki kusema kwamba Bw Mugabe alikubaliana nami kabisa,” alisema Askofu Welby.

Mkutano huo wa faraghani ulifanyika mjini Harare, baada ya Askofu Welby, ambaye yumo katika taifa jirani la Zambia anakohudhuria mkutano wa viongozi wa kanisa la Kiangilikana kufanya ziara fupi Zimbabwe.

Msemaji wa Lambeth Palace amesema mpango huo ulipangwa dakika za mwishomwisho na ulidumu chini ya saa moja.

Bw Mugabe ni Mkatoliki na hupinga sana ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Askofu Welby amesema Bw Mugabe hakukubaliana naye kabisa
Maafisa wa kanisa hilo wamesema mkutano huo ulikuwa sana wa kidini badala ya kisiasa ingawa uhusiano baina ya serikali na kanisa ulijadiliwa.

Chanzo BBCswahili

Magufuli ataka daraja lipewe jina la Nyerere

Daraja la kigamboni lina urefu wa mira 680
Rais wa Tanzania John Magufuli amependekeza daraja mpya la Kigamboni lipewe jina la mwanzilishi wa taifa hilo Mwalimu Julius Nyerere.

Akiongea muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi daraja linafaa kupewa jina la Mwalimu Julius Nyerere kutokana na mchango wake kwa nchi hiyo.

Daraja la Kigamboni lilianza kutumika tarehe 16 Aprili, 2016 na lina urefu wa mita 680 na barabara unganishi upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilomita 2.5.
Rais Magufuli baada ya kuzindua daraja la Kigamboni
 Ujenzi wake ulifanywa na kampuni ya China Railway 15 Group ikishirikiana na kampuni ya China Bridge Engineering Group.

Daraja hilo ndilo la kwanza la kubeba uzito wa barabara kwa kutumia nyaya Afrika Mashariki na la tatu Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara bila kuhesabu Afrika Kusini.

Linamilikiwa na serikali ya Tanzania na Hazina ya Malipo ya Uzeeni (NSSF) kwa 40% na 60% mtawalia na litachukua nafasi ya feri ya MV Magogoni.
Wenye magari watalipia kutumia barabara hiyo
 Wenye magari na pikipiki watahitajika kulipa kutumia daraja hilo lakini wapitanjia watavuka bila malipo.

Ujenzi wa daraja hilo, ambao uligharimu dola 128 milioni za Kimarekani, ulianza mwaka 2012.

Chanzo BBCswahili.